Mkaazi wa Dar es Salaam asema Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar ni bora duniani
Wakati Tanzania ikiadhimisha siku ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, uliotimiza miaka 60 Ijumaa, Rais Samia Suluhu Hassan amewataka vijana nchini humo kuuenzi na kuulinda muungano.
Wakati huo huo vijana katika maadhimisho hayo wameitaka serikali kuwapatia elimu juu ya Muungano ili kuwasaidia kuufahamu kwa undani pamoja na kutatua changamoto zilizopo.
Sherehe za Muungano zimefanyika Jijini Dar es Salaam katika Uwanja wa Uhuru na kuhudhuriwa na Marais kutoka nchi 7 za Afrika ikiwemo Kenya, Burundi, Zambia, Somalia, Comoro na Namibia. Pia imehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Kiserikali kutoka Barani Afrika.
Wakati akilihutubia taifa Rais Samia amewahimiza vijana kuulinda na kuuenzi Muungano kwa kuwa ni urithi na tunu ya Taifa la Tanzania na ni tunu ya Afrika kwa ujumla.
“Matokeo ya Sensa ya mwaka 2022 yanatuonyesha kwamba idadi kubwa ya Watanzania ni vijana kwa kuzingatia hilo uimara na uendelevu upo mikononi mwa vijana. Nina wasihi sana vijana wote wa Tanzania muwe walinzi wa Muungano huu,” alisema Rais Samia.
Hata hivyo bado vijana wamekuwa wakilalamika ukosefu wa elimu ya Muungano ambayo ilipaswa kutolewa ili kuwasaidia kufahamu haki zao na pia kufahamu mipaka yao katika muungano huo.
#Maadhimisho #muungano #zanzibar #tanganyika #voa #voaswahili #raiswatanzania #samiasuluhuhassan #JuliusNyerere #abeidamanikarume
11 May 2024
- Kenyans are currently paying a 1.5% housing levy and gearing up for a 2.5% health insurance contribution.
11 May 2024
- Kenyans.co.ke takes a look at five taxes and how they will affect the taxpayer.
11 May 2024
- The weatherman also projected how weather in Nairobi is expected to behave.
12 May 2024
- The official death toll from devastating flash floods in northern Afghanistan has risen to 153 people across three provinces, the Taliban's interior ministry said on Saturday, while the World Food Programme said it was double that.
12 May 2024
- Five people were killed and nine wounded in three separate Ukrainian drone and artillery strikes on the Russian border provinces of Belgorod and Kursk, and the city of Donetsk, which Russia claims to have annexed, local officials said on Saturday.
12 May 2024
- Israel called on Saturday for Palestinians in more areas of Gaza's southern city of Rafah to evacuate and head to what it calls an expanded humanitarian area in Al-Mawasi, in a further indication that the military is pressing ahead with its plans for a…
12 May 2024
- Fresh outlook needed to transform parastatals
12 May 2024
- Why CS Linturi should resign or just be fired
12 May 2024
- What strategic leadership entails and how to win citizens' goodwill
12 May 2024
- Mother's Day: The unsung heroines amid raging floods
12 May 2024
- Ex-civil servants to earn more if MPs pass changes to pensions law
12 May 2024
- Kill or keep our parties? The dilemma facing Mudavadi and Wetang'ula
12 May 2024
- Mombasa locals living in fear after dreaded youthful gangs strike again