- 6,221 viewsDuration: 45sFamilia ya John Waruingi Kamau inaishi na mahangaiko ya kumtafuta mwana wao ambayealitoweka mwezi uliopita na hadi sasa hajulikani alipo. John mwenye umri wa miaka 26 na mwenye kimo cha takriban futi 5 na inchi 9, alionekana Mara ya mwisho siku ya Jumatano, tarehe 12 mwezi Novemba mwaka huu wa 2025, huko Kikuyu.Yeyote aliye na taarifa kuhusu alipo anaombwa kuwasiliana na familia yake kupitia nambari ya simu 0735 823 772, au kutoa taarifa katika kituo cha polisi kilicho karibu.