- 193 viewsDuration: 1:41Wafugaji na wakulima katika kaunti ya Tana River sasa watakuwa wanapokea jumbe za tahadhari za mapema kupitia simu zao za rununu ili kujiandaa vilivyo na athari za mafuriko ama kiangazi. Akizindua awamu ya pili wa mradi wa Wiser - Kenya, msimamizi wa mradi huo Philip Omondi amesema hatua hii itapunguza hasara ya kila mwaka ya kupoteza mifugo na mimea nyakati za ukame na mafuriko. Alisema wafugaji pia wataweza kuhifadhi chakula na maji ya mifugo wao kwa matumizi ya siku za kiangazi.