Kamati ya bunge la taifa kuhusu ulinzi, ujasusi na mahusiano ya kigeni imehitimisha shughuli ya kuwasaili watu wanne waliopendekezwa kuwa mabalozi huku mzozo huko Goma katika jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ukishamiri kwenye mchakato huo wa usaili. Jamhuri ya DRC iliyopinga rasmi kupelekwa kwa mkuu wa ubalozi mdogo wa Kenya jijini Goma, wasiwasi wa kiusalama nchini Haiti, usalama wa wakimbizi kutoka Kenya katika eneo hilo linalokumbwa na mzozo na maswala ya leba katika eneo la Ghuba pia yaliangaziwa kwenye vikao hivyo.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive