Russia iliionya Marekani kabla ya kufyatua kombora la Oreshnik
Msemaji wa Kremlin amesema leo Ijumaa kwamba Moscow iliipelekea Marekani onyo dakika 30 kabla ya kufyatua kombora jipya la masafa ya kati huko Ukraine.
Kremlin iliruhusu kufyatuliwa kombora hilo jipya lililopewa jina la Oreshnik dhidi ya mji ulio kati kati mwa Ukraine wa Dnipro jana alhamisi.
Rais Putin amesema kwenye hotuba yake kwamba shambulio hilo limefanyika kujibu hatua ya Kyiv wiki hii kutumia makombora ya Marekani na Uingereza yenye uwezo wa kufika mbali ndani ya Russia.
Putin alionya kwamba mfumo wa Marekani wa ulinzi wa anga hautaweza kuzuia kombora jipya ambalo anasema lina safiri kwa kasi ya mara 10 zaidi ya sauti.
Hii leo pia msemaji Peskov aliulaumu utawala wa hivi sasa wa Marekani kwa kuzorotesha ugomvi wa Ukraine na kusema kwamba hakuna mawasiliano kati ya Moscow na Washington juu ya suala hili. - AP
Wakati huo huo Waziri wa ulinzi wa Ukraine Rustem Umerov amesema serikali yake ilikuwa inaongeza uwezo wa ulinzi wa anga wakati ikijibu mashambulizi ya makombora ya masafa marefu ya Russia katika mji wa ukarine wa Dnipro.
Umerov ameyasema hayo leo katika maelezo yake kwa vyombo vya habari akiwa na mwenzake wa Sweden Pal Johnson mjini Stockholm.
Jonson ameongeza kuwa shambulizi la Russia haliwezi kuikatisha tamaa uungaji mkono wa serikali yake kwa Ukraine.
Alhamisi Russia ilifyatua makombora ya masafa marefu kujibu hatua ya Marekani na Uingereza kuiruhusu Kyiv kushambulia ndani ya ardhi ya Russia na silaha zake za Magharibi za ubora wa juu.
- AP and Reuters
#voaswahili #afrika #ukraine #russia #kombora #oreshnik #dnipro #moscow #russia
17 Jun 2025
- Gachagua has torn into President Ruto for what he terms as a disregard for human life.
17 Jun 2025
- The mask vendor was unarmed and shot in full glare of the public.
17 Jun 2025
- One person was shot by police at point-blank range, amid allegations police turned a blind eye to armed goons who attacked protesters.
18 Jun 2025
- The gunmen attacked after dark and chased farmer Fidelis Adidi away from the central Nigerian village of Yelwata. The next morning, he returned to find the charred remains of one of his two wives and four of his children.
18 Jun 2025
- Togo has suspended broadcasts of French state-funded international news outlets RFI and France 24 for three months, its communications authority said on Monday, accusing them of a lack of impartiality and rigour.
18 Jun 2025
- Russia launched dozens of drones and missiles at Kyiv in the early hours of Tuesday, killing at least 10 people and wounding dozens of others, as negotiations faltered between Kyiv and Moscow.
18 Jun 2025
- Detectives investigating the murder of blogger Albert Ojwang’ were yesterday sifting through the call data records (CDR) to establish any possible communication between Deputy Inspector General of Police Eliud Lagat and the officers linked to the death…
18 Jun 2025
- The Senate and the National Assembly have, for the third time, failed to agree on equitable revenue sharing for county governments in the 2025-26 financial year, with both houses maintaining hardline stances during ongoing mediation. During the June 17…
18 Jun 2025
- A group of former political prisoners has called on Raila Odinga’s opposition faction to withdraw from the broad-based government, arguing this would pave the way for forming a new administration. The group – including prominent figures such as Oginga…
18 Jun 2025
- CAK eyes forensic lab, stricter laws to enhance consumer protection
18 Jun 2025
- From pitching tents to the sought-after events planner
18 Jun 2025
- Treasury PS: State to automate debt servicing processes
18 Jun 2025
- How police have turned cells into death traps for leaders' 'enemies'