Angola yasema itajaribu kusimamia mazungumzo kati ya DRC na M23
Angola imesema siku ya Jumanne itajaribu kusimamia mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda katika siku zijazo.
Haikufahamika iwapo serikali ya Congo, ambayo ilikataa mara nyingi kufanya mazungumzo na M23, itashiriki katika mazungumzo hayo.
Msemaji wa ofisi ya rais wa Congo aliiambia Reuters mamlaka hiyo imezingatia hatua hiyo, wakati naibu msemaji wa M23 alisema ulikuwa “ni ushindi wa hoja” na kuthibitisha ushiriki wa kikundi hicho katika mazungumzo hayo.
Rais wa DRC Felix Tshisekedi alifanya ziara ya kikazi mjini Luanda na alikutana na mwenzie Joao Lourenco, ofisi ya rais wa Angola ilisema katika taarifa kwenye Facebook.
“Angola kama mpatanishi katika mzozo wa mashariki mwa Congo, itaanzisha mawasiliano na M23, ili wajumbe kutoka Congo na M23 wafanye mazungumzo ya moja kwa moja mjini Luanda katika siku zijazo,” ofisi ya rais iliongeza.
Nchi hiyo iliyoko Kusini mwa Afrika imekuwa ikijaribu kusimamia kufikiwa kwa sitisho la mapigano na kupunguza mivutano kati ya Congo na jirani yake Rwanda, ambayo imekuwa ikishutumiwa kuwasaidia kikundi cha waasi wa Kitutsi.
Rwanda imekanusha kuwapa msaada wa silaha na wanajeshi waasi wa M23, na imesema majeshi yake yanajihami dhidi ya jeshi la Congo na wanamgambo wenye chuki na Kigali.
Waasi wa M23 wamekamata miji mikubwa miwili iliyoko mashariki mwa Congo tangu Januari katika mvutano wa mgogoro wa muda mrefu ambao kiini chake ulisambaa Congo kutokana na mauaji ya halaiki ya Rwanda yam waka 1994 na juhudi ya kutaka kudhibiti eneo kubwa lenye madini nchini Congo.
#angola #waasi #m23 #congo #felixtshisekedi #JoaoLourenco #rwanda
30 Apr 2025
- Suspects of different nationalities came together to defraud victims.
30 Apr 2025
- Ruto's surprise appearance at the Vatican despite sending Wetangula caused a buzz online.
30 Apr 2025
- The MCA is part of the numerous residents that have been the latest targets.
30 Apr 2025
- Kenya’s revised foreign policy is designed to address the interests of citizens and reposition Kenya's foreign engagements on the dynamic global landscape, Prime Cabinet Secretary Musalia Mudavadi has said.
30 Apr 2025
- President William Ruto’s State Visit to China saw more than 20 trade agreements and memoranda of understanding signed, that aim at improving various sectors of the economy.
30 Apr 2025
- The Climate Reality Project, a climate-focused nonprofit founded by former U.S. Vice President Al Gore, is set to host an in-person training event in Nairobi in June.
30 Apr 2025
- President William Ruto has praised the increased contributions to the National Social Security Fund (NSSF) as a step toward the country’s financial security.
30 Apr 2025
- Hungary's Foreign Minister presented a bill to the National Assembly proposing Hungary's formal withdrawal from the ICC.
30 Apr 2025
- Suspects of different nationalities came together to defraud victims.
30 Apr 2025
- According to the University’s Vice Chancellor Prof Deogratius Jaganyi, the program dubbed as Africa meets Bavaria, is aimed at fostering a vibrant research culture among students.
30 Apr 2025
- Ruto congratulated Chitunga and assured him of government support.
30 Apr 2025
- Ruto's surprise appearance at the Vatican despite sending Wetangula caused a buzz online.
30 Apr 2025
- According to lawmakers, while the volume of money staked by punters has been steadily rising,reflected in a sharp increase in excise duty collections, taxes from winnings have paradoxically declined.