Angola yasema itajaribu kusimamia mazungumzo kati ya DRC na M23
Angola imesema siku ya Jumanne itajaribu kusimamia mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda katika siku zijazo.
Haikufahamika iwapo serikali ya Congo, ambayo ilikataa mara nyingi kufanya mazungumzo na M23, itashiriki katika mazungumzo hayo.
Msemaji wa ofisi ya rais wa Congo aliiambia Reuters mamlaka hiyo imezingatia hatua hiyo, wakati naibu msemaji wa M23 alisema ulikuwa “ni ushindi wa hoja” na kuthibitisha ushiriki wa kikundi hicho katika mazungumzo hayo.
Rais wa DRC Felix Tshisekedi alifanya ziara ya kikazi mjini Luanda na alikutana na mwenzie Joao Lourenco, ofisi ya rais wa Angola ilisema katika taarifa kwenye Facebook.
“Angola kama mpatanishi katika mzozo wa mashariki mwa Congo, itaanzisha mawasiliano na M23, ili wajumbe kutoka Congo na M23 wafanye mazungumzo ya moja kwa moja mjini Luanda katika siku zijazo,” ofisi ya rais iliongeza.
Nchi hiyo iliyoko Kusini mwa Afrika imekuwa ikijaribu kusimamia kufikiwa kwa sitisho la mapigano na kupunguza mivutano kati ya Congo na jirani yake Rwanda, ambayo imekuwa ikishutumiwa kuwasaidia kikundi cha waasi wa Kitutsi.
Rwanda imekanusha kuwapa msaada wa silaha na wanajeshi waasi wa M23, na imesema majeshi yake yanajihami dhidi ya jeshi la Congo na wanamgambo wenye chuki na Kigali.
Waasi wa M23 wamekamata miji mikubwa miwili iliyoko mashariki mwa Congo tangu Januari katika mvutano wa mgogoro wa muda mrefu ambao kiini chake ulisambaa Congo kutokana na mauaji ya halaiki ya Rwanda yam waka 1994 na juhudi ya kutaka kudhibiti eneo kubwa lenye madini nchini Congo.
#angola #waasi #m23 #congo #felixtshisekedi #JoaoLourenco #rwanda
15 Jun 2025
- Complications emerged with the protocol of official functions during Ruto and Gachagua's tenure.
15 Jun 2025
- For some people, being alongside trickling water masses initiates the urge.
15 Jun 2025
- The president also issued a warning to other contractors.
15 Jun 2025
- In a statement posted on his official X account on Sunday, Kindiki acknowledged Kalonzo's decision to decline his invitation to work with the government, saying he respected it—but issued a stern warning against what he called "unprovoked falsehoods."
15 Jun 2025
- The deceased, identified as Calvince Omondi Onditi, was apprehended by the area chief at around 3 a.m. on Sunday after reportedly being found in a goat pen in a homestead near Ndhuru Trading Centre.
15 Jun 2025
- The President said the government, in partnship with the World Bank, will provide KSh50,000 to 70 small business owners - a total of KSh3.5 million - in each of the country’s 1,450 wards.
15 Jun 2025
- Speaking on Sunday during a Church Service at AIC Nairagie Enkare in Narok East, Narok County, the DP encouraged citizens to be patriotic and peacefully co-exist for the nation to prosper.
15 Jun 2025
- National Assembly Speaker Moses Wetang'ula says construction of key roads in the western region that are stalled is set to resume the new Financial Year, 2025/26.
15 Jun 2025
- Officials from the U.S. National Transportation Safety Board (NTSB) surveyed the site of Air India plane crash that killed at least 271 people, sources said on Sunday, with families continuing to wait for DNA profiling results to identify charred bodies.
15 Jun 2025
- A 26-year-old woman is in police custody after attempting to smuggle cocaine outside the country through the Jomo Kenyatta International Airport (JKIA).
15 Jun 2025
- Complications emerged with the protocol of official functions during Ruto and Gachagua's tenure.
15 Jun 2025
- Ojwang's death sparked protests, particularly in Nairobi, with demonstrators demanding answers
15 Jun 2025
- Vigils honouring the dead have taken place across India and the UK