- 2,994 viewsDuration: 2:48Kundi la kutetea haki za binadamu la Vocal Africa limetishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) na Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) kwa kushindwa kuchukua hatua dhidi ya maafisa waliokiuka sheria za uchaguzi. Kundi hilo linasisitiza kuwa uchaguzi mdogo uliokamilika haukuwa huru wala wa haki kutokana na visa vingi vya ghasia, vitisho, na hongo kwa wapiga kura.