Rais William Ruto ameridhia ombi la kuupa jina jipya uwanja wa michezo wa Talanta kuwa uwanja wa michezo wa kimataifa wa Raila Odinga. Rais Ruto katika hotuba yake mnamo Ijumaa, alipoliongoza taifa kusherehekea sikukuu ya 62 ya jamhuri, alisisitiza kwamba uwanja huo mpya unaoendelea kujengwa utapewa jina la marehemu Raila Odinga. Aidha rais Ruto aliahidi kukarabati miundomsingi ya barabara za jiji ukiwemo ujenzi wa safu mbili za barabara kila upande wa barabara ya Rongai Kiserian pamoja na barabara ya moja kwa moja kwenye barabara kuu ya Thika.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive