- 4,369 viewsDuration: 1:27Mwenyekiti wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini Caleb Kositany amewarai wakaazi wa webuye kudumisha usalama katika mchakato mzima wa kuanzishwa kwa safari za ndege eneo hilo. Akizungumza baada ya kukagua uwanja wa ndege wa Matulo, Kositany amesema Mamlaka ya viwanja vya ndege itaharakisha utekelezaji wa miradi muhimu ya miundo mbinu ili kuufanya uwanja huo kuanzisha safari za ndege. Aidha gavana wa bungoma, Kenneth Lusaka amesema serikali ya kaunti iko tayari kushirikiana na mamlaka hiyo ili kufanikisha mradi huo. Tayari kaunti imetambua ardhi inayohitajika kwa ajili ya upanuzi wa uwanja huo na inaendelea kushirikiana na wakazi watakaoathirika kuhusu mipango ya fidia.