- 289 viewsDuration: 1:15Baadhi ya viongozi kutoka kaunti ya Garissa sasa wanataka serikali kuweka mikakati na kuongeza juhudi za kutoa msaada kwa waathiriwa wa njaa wakisema hali inazidi kuwa mbaya. Viongozi hao wanadai kuwa wakongwe, kina mama na watoto ndio walioathirika pakubwa kwenye janga hili na kuhimiza mashirika mengine kusaidia kwa kutoa chakula na maji.Aidha serikali ya kaunti hiyo imetakiwa kuhamasisha wafugaji kuanza kuuza mifugo wao mapema ili kuepuka hasara.