- 1,041 viewsDuration: 3:01Uratibu wa mipaka nchini unaofaa kuandaliwa kabla ya uchaguzi mkuu kisheria unazidi kuipiga chenga tume ya uchaguzi IEBC, kutokana na changamoto za kisheria. Mwenyekiti wa tume hiyo Erastus Ethekon amesema kuwa utata kuhusu sensa umetatiza kufanyika kwa shughuli hiyo huku kesi ikiendelea. Ethekon amesema kuwa uratibu wa mipaka utafanywa kwa awamu japo hakuna maeneo bunge yatakayoongezwa.