Mahakama imewaelekeza wahusika katika mgogoro wa muda mrefu wa udhibiti wa Kampuni ya Directline Assurance, kufikia makubaliano kuhusu ni maombi yapi kati ya mengi yaliyowasilishwa yatajumuishwa. Jaji Francis Gikonyo akisema hii itasaidia kesi hiyo kulekezwa katika masuala ya msingi ya uongozi na umiliki wa hisa. Akizungumza Jumanne wakati wa kutajwa kwa ombi la kupuuza mahakama dhidi ya mwenyekiti wa Royal Credit Limited, Dkt. SK Macharia, Jaji Gikonyo amesema kuwa maombi mengi yamemekuwa yakichelewesha kesi ambayo ilipaswa kuwa tayari imekamilika