- 2,332 viewsDuration: 2:38Wafanyakazi wa Jua Kali wanaoshiriki katika mradi wa ujenzi wa Nyumba za Bei Nafuu eneo la Shauri Moyo jijini Nairobi wameeleza wasiwasi wao kuhusu kucheleweshwa kwa malipo, pamoja na upungufu wa vifaa vya kazi. Kwa mujibu wa wafanyakazi hao, mafundi wamepokea malipo kiasi, lakini wachoraji wanasema hawajalipwa kwa muda wa wiki mbili sasa licha ya kuendelea kufanya kazi. Wanasema makubaliano ya awali yalikuwa kuwa mishahara itolewe kila wiki. Aidha, wameripoti kuwa vifaa vya ujenzi havitoshi, hali inayochelewesha kazi na kuwafanya wafanye kazi kwa ugumu zaidi. Wasimamizi wa mradi waliwaahidi kmalipo leo, lakini hakuna malipo yaliyokuwa yametolewa kufikia wakati wa kwenda hewani.