- 135 viewsDuration: 1:39Matumaini mapya yameanza kuchomoza kwa wakazi wa Lokesheni ya Kamoi katika Eneo Bunge la Keiyo Kaskazini, Kaunti ya Elgeyo Marakwet, baada ya ukarabati wa bwawa la maji la Sing’ore . Ukarabati huo unahusisha kuondoa tope na kuanza kusambaza maji safi ya matumizi ya nyumbani na kwa ajili ya unyunyiziaji mashamba. Mradi huo yenye thamani ya shilingi milioni 80 unatarajiwa kunufaisha zaidi ya wakazi 3,000 utakapokamilika ndani ya miezi 10 ijayo.