- 241 viewsDuration: 2:54Gavana wa Busia Paul Otuoma ameandikisha taarifa na tume ya kupambana ufisadi, kufuatia uchunguzi wa kesi ya utoaji zabuni ya shilingi bilioni 1.4 kinyume cha sheria. Katika uchunguzi huo, jumla ya kampuni ishirini na sita zinazohusihwa na wendani wa karibu wa maafisa wakuu wa serikali ya kaunti ya Busia zinadaiwa kupokea fedha hizo. Gavana Otuoma amesema yuko tayari kushirikiana na EACC ili kubaini mbivu na mbichi kuhusu madai ya ufisadi katika kaunti hiyo