- 322 viewsDuration: 2:13Wizara ya biashara imeanza kupokea maoni kutoka kwa wafanyabiashara wa Garissa kuhusu mswada wa kitaifa wa maendeleo ya biashara wa mwaka wa 2025 ambao unalenga kuondoa vikwazo vingi kwenye sekta hiyo. Kwenye kikao hicho, wafanyabiashara hao walilalamikia idadi ya vizuizi barabarani vinavyotoza ushuru hatua inayosababisha mazingira ya kufanyia biashara kuwa magumu zaidi.