- 6,242 viewsMwanamume mmoja leo nusura akatize hotuba ya rais ruto huko wajir baada ya kujaribu kumkimbilia rais jukwaani. Mlinzi wa rais hata hivyo alifanikiwa kumrukia jamaa huyo kabla hajamfikia rais ambaye kwa sekunde chache alilazimika kukatiza hotuba yake. Rais hata hivyo akiwaagiza walinzi wake kumruhusu kufuatilia yaliokuwa yakiendelea katika hafla ya mradi wa nyota huko Wajir.