- 2,669 viewsDuration: 1:36Kinara wa chama cha Wiper Patriotic Front, Kalonzo Musyoka, anashinikiza ukame utangazwe kuwa janga la kitaifa ili kuvutia msaada zaidi. Kalonzo amesema kuwa ukame ni jambo la dharura na linahitaji kuingiliwa kati haraka ili kuzuia maafa ya binadamu na mifugo. Kinara huyo wa WPF amesema kuwa atawahusisha wadau wa kimataifa na wa humu nchini ili kutafuta msaada kwa familia zilizoathirika. kadhalika kalonzo ameitaka IEBC kuweka vituo zaidi vya kupiga kura kwa wakenya wanaoishi ughaibuni na vilevile kuitaka serikali kuwasaidia wakenya wanaotaabika katika mataifa za nje. Kalonzo aliwasili jana kutoka mjini Washington DC, Marekani.