- 338 viewsDuration: 3:38Msitu wa Mlima Elgon ni hazina ya kitaifa inayobeba historia, uhai na mustakabali wa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo. Wanaharakati wa mazingira wameanzisha mikakati ya kulinda na kuhamasisha umma kuhusu umuhimu wa kutunza msitu wa Mlima Elgon, ambao si tu hifadhi ya kitaifa ya wanyama pori bali pia ni mojawapo ya nguzo saba za chemchemi za maji nchini. Hata hivyo, kuna wasiwasi unaoongezeka kuhusu uharibifu wa msitu huo na hatari ya kupotea kwa turathi hiyo adhimu.