- 18,153 viewsDuration: 2:59Mtu mmoja amethibitishwa kufariki kufuatia vurugu zilizoshuhudiwa mjini Mbale, Vihiga saa chache kabla ya mkutano wa linda mwananchi unaoongozwa na seneta wa Nairobi Edwin Sifuna. Marehemu alivamiwa na umati baada ya kudaiwa kumdungwa kisu jamaa aliyehamia mrengo tofauti. Haya yakijiri Mbale, kule kakamega njama ya kutibua mkutano katika uwanja wa amalemba ulizimwa baada ya Sifuna kuwahimiza wafuasi wasiondoke uwanjani licha ya vitoa machozi kutupwa katikati ya umati mkutano ulipokuwa ukiendelea