- 6,032 viewsDuration: 2:04Wakazi wa kijiji cha Shivakala–Lusokho eneo bunge la Tongaren kaunti ya Bungoma wameshangazwa na tukio moja ambapo jamaa wa miaka 21 anadaiwa kumuuwa nduguye wa miaka 24 kufuatia mzozo kuhusu viatu aina ya gumboots. Kulingana na mama yao, ugomvi ulipozuka kati ya wawili hao, mwanawe Joshua Wafula alidungwa kisu mara kadhaa na nduguye David Wanyonyi na kisha kufariki muda mfupi baadaye...Naibu Chifu wa eneo hilo Fred Wanyonyi alithibitisha tukio hilo akisema mshukiwa tayari amekamatwa huku uchunguzi ukiendelea..