- 192 viewsDuration: 1:39Zaidi ya wanafunzi mia mbili mayatima katika kaunti ya Vihiga wana sababu ya kutabasamu baada ya kupokea ufadhili wa karo wa shilingi milioni 5. Akizungumza katika hafla hiyo, Mwakilishi wa kike kaunti hiyo Beatrice Adagala ameitaka serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ya NGCDF kwa kaunti zote nchini akisema pesa wanazopokea hazitoshi kukabili changamoto katika kaunti hizo. Aidha Wazazi wanataka serikali kurudisha bima ya afya kwa wanafunzi ili kuepuka changamoto zaidi.