- 191 viewsDuration: 2:05Zaidi ya wanafunzi 200 wameshiriki mashindano ya kusoma Quran huko Nyali kaunti ya Mombasa. Waandalizi wa mashindano hayo wanasema hatua hiyo ni ya kuwataka vijana kujukumika wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhan. Viongozi wa kidini kwa upande wao wametaka vijana zaidi kujitokeza katika mashindano haya ili kuepuka kujiunga na makundi ya kihuni. Mashindano hayo yaliofanyika katika ukumbi wa Freer Town yameendelea kuvutia wahisani huku raundi ya tatu ikitarajiwa kabla ya mwezi mtukufu wa ramadhan kukamilika.