- 194 viewsDuration: 2:03Kongamano la wanawake lililoandaliwa hapa jijini nairobi liliwaleta pamoja viongozi wa kanisa na wanajamii kujadili nafasi ya mwanamke katika safari ya maendeleo ya Kenya. Waziri wa Jinsia Hannah Cheptumo aliwahimiza wanawake kuhakikisha wamenufaika na miradi ya serikali, hususan mpango wa nyumba za bei nafuu, kama njia ya kujitegemea kifedha na kuimarisha familia. kina mama kutoka pembe mbalimbali za nchi walikusanyika jijini Nairobi kwa mkutano huo ulioandaliwa na Kanisa la AIC.