- 689 viewsDuration: 2:31Msimamizi wa bajeti za serikali Margaret Nyakang’o aliibua maswali kuhusu safari nyingi za waakilishi wadi na serikali za kaunti. Ripoti yake ikionyesha ubadhirifu mkubwa wa mali ya umma kwenye safari hizo, ambazo nyingi hazina umuhimu kwa mlipa ushuru. Na kama anavyoarifu emmanuel too, kaunti ya nairobi inaongoza kwa safari hizo, ikitumia zaidi ya shilingi milioni 800 kwenye safari za ughaibuni na hapa nchini, katika mwaka wa kifedha uliopita.