- 387 viewsMajeshi ya Ukraine yameishambulia meli ya Russia iliyokuwa inawasili Crimea, shambulizi lililopiga sehemu ya meli kadhaa za Russia zilizoko katika bahari ya Black Sea ambazo jeshi la anga la Ukraine lilisema zinashukiwa kubeba droni zilizotengenezwa Iran. Wizara ya Ulinzi ya Russia ilisema kuwa shambulizi lililofanywa na Ukraine liliharibu meli ya Novocherkassk katika kituo cha Feodosia. Sergei Aksyonov, gavana wa Crimea aliyewekwa na Russia, alisema kupitia mtandao wa Telegram shambulizi hilo liliuwa mtu mmoja na kujeruhi wengine wawili. Mashirika ya habari ya Russia yaliripoti kuwa Rais Vladimir Putin alipewa muhtasari wa shambulizi hilo. Jeshi la anga la Ukraine lilisema limetumia makombora ya masafa marefu na kuwa shambulio hilo liliiteketeza meli hiyo. Kamanda wa jeshi la anga la Ukraine Mykola Oleshchuk alisambaza video kupitia mtandao wa Telegram ikionyesha mlipuko mkubwa huko Feodosia. “Na meli za Russia zinazidi kupungua zaidi,” Oleshchuk alisema. Jeshi la Ukraine pia limeripoti Jumanne kuangusha droni 13 kati ya 19 ambazo zilitumiwa na Russia kufanya mashambulizi usiku kucha. Lilisema droni hizo ziliangushwa huko katika mikoa ya Odesa, Kherson, Mykolaiv na Khmelnytskyi Russia ilidai Jumatatu kuwa majeshi yake yalikuwa yameteka mji wa kimkakati wa Maryinka ulioko mashariki mwa Ukraine, lakini Kyiv ilikanusha dai hilo, ikiripoti kuwa majeshi yake yalizima “mashambulizi matatu yaliyofeli” karibu na jamii ambayo imeharibiwa na kutelekezwa. “Si sahihi kuzungumzia kuiteka Maryinka,” msemaji wa jeshi la Ukraine Oleksandr Shtupun alikiambia kituo cha televisheni cha Ukraine kufuatia madai ya Waziri wa Ulinzi wa Russia Sergei Shoigu wakati wa mkutano wake na Rais Vladimir Putin ulioonyeshwa kupitia televisheni. “Mapigano yanaendelea huko Maryinka,” Shtupun alisema. “Hivi sasa, wanajeshi wetu wako katika maeneo ya utawala ya mpakani huko Maryinka, lakini mji huo umeangamizwa kabisa,” alisema. Waliochangia katika ripoti hii ni Radio Free Europe/Radio Liberty Baadhi ya taarifa katika ripoti hii zinatokana na mashirika ya habari ya Associated Press, Agence France-Presse and Reuters. #rais #vladimirputin #uhaini #wagner #usaliti #russia #joebiden #marekani #wagnergroup
Ukraine yaharibu meli kadhaa za Russia kwa makombora ya masafa marefu
- - Citizen TV Live ››
- - Citizen TV Live ››
- - Citizen TV Live ››
- - Citizen TV Live ››
- - Citizen TV Live ››
- - Citizen TV Live ››
- - Citizen TV Live ››
- - Citizen TV Live ››
- - Citizen TV Live ››
- 16 Aug 2025 - Wiper party leader Kalonzo Musyoka has accused President William Ruto of stifling the freedom of the Judiciary and right of citizens to political association in recent government crackdowns that target dissent.
- 16 Aug 2025 - President William Ruto has called on Harambee Stars fans to maintain discipline during the team's Sunday match against Zambia at the Kasarani Stadium in Nairobi.
- 16 Aug 2025 - The African Union has backed a campaign to end the use by governments and international organisations of the 16th-century Mercator map of the world in favour of one that more accurately displays Africa's size.
- 16 Aug 2025 - China urged Cambodia and Thailand to continue efforts towards restoring a lasting peace at their border as soon as possible, a Chinese foreign ministry statement said on Friday as it summarised an earlier trilateral meeting.
- 16 Aug 2025 - Mali's military-led government has arrested two generals and a French national, accusing them of participating in an alleged plot to destabilise the West African nation, according to a government statement and state-owned media.
- 16 Aug 2025 - Indonesia will launch a broader crackdown on the illegal exploitation of natural resources after a survey found that palm plantations on 3.7 million hectares (14,300 square miles) were operating in violation of the law, President Prabowo Subianto said…
- 16 Aug 2025 - U.S. President Donald Trump’s administration is discussing a refugee admissions cap of around 40,000 for the coming year with a majority allocated to white South Africans, according to two U.S. officials briefed on the matter and an internal refugee…
- 16 Aug 2025 - Government and civil service should have been doing this for 12 years. Now five people will recommend solutions based on Nadco’s imperfect proposals?
- 16 Aug 2025 - “A total of 1,100 registered groups from Nairobi submitted proposals for their empowerment programmes or projects, all approved, all funded, all received,” he stated in a post.
- 16 Aug 2025 - Enock Andanje collapsed and died on Friday while attending a widows’ empowerment event.