Hofu ya janga la kibinadamu yaongezeka Gaza
Umoja wa mataifa Jumanne ulionya dhidi ya mashambulizi ya ardhini huko Rafah katika Ukanda wa Gaza, ukisema mashambulizi hayo yanaweza kusababisha mauaji makubwa katika eneo hilo la kusini mwa Palestina ambako zaidi ya watu milioni 1 wanaishi.
Israel imesema inataka kuwaondoa wanamgambo wa Hamas kwenye maficho yao huko Rafah na kuokoa mateka wa Israel wanaoshikiliwa na Hamas, na inaandaa mipango ya kuwaondoa raia wa Palestina waliokwama huko.
“Operesheni za kijeshi huko Rafah zinaweza kusababisha mauaji makubwa huko Gaza. Zinaweza pia kukwamisha shughuli za kutoa misaada ya kibinadamu ambazo tayari zilikuwa zimedhoofika,” alisema mkuu wa misaada ya kibinadamu kwenye Umoja wa mataifa Martin Griffiths.
Alisema katika taarifa kwamba “Jumuia ya kimataifa imekuwa ikionya dhidi ya athari mbaya za mashambulizi ya ardhini huko Rafah, na serikali ya Israel haiwezi kuendelea kupuuza wito wa Jumuiya ya Kimataifa.
Mazungumzo yanayojumuisha Marekani, Misri, Israel na Qatar kuhusu sitisho la mapigano Gaza yalimalizika Jumanne bila kupiga hatua yoyote huku shinikizo likiongezeka kwa Israel kuachana na mpango wake wa kuishambulia Rafah.
Wakati huo huo Al-Tikeye taasisi ya hisani yenye makao yake Rafah inaendelea kuwalisha Wapalestina wengi wao watoto na wanawake wanaokabiliwa na njaa waliokoseshwa makazi katika mji ulioko upande wa kusini wa Ukanda wa Gaza.
Kwa mujibu wa wizara ya afya Gaza inayoendeshwa na Hamas mashambulizi ya angani na ardhini yanayofanywa na Israel yameuwa watu zaidi ya 28,000 na kujeruhi zaidi ya wengine 65,000 katika eneo finyu la Gaza.
Mashambulizi haya yalianza Oktoba 7 kufuatia mauaji ya Oktoba 7 huko kusini mwa Israel, yaliofanywa na wanamgambo kutoka Gaza waliouwa takriban watu 1,200 na kuwateka watu 250. - AP
#Haifa #waelaldahdouh #hamzaaldahdouh #shirikalamwezimwekundu
#Rafah #Netanyahu #Misri #Hamas #Gaza #Palestina #IDF #GalMeirEizenkot #mauaji #jeshi #israel #voa #voaswahili #mwandishi #aljazeera #maghazi #wahouthi #marekani #uingereza #shambulizi #dhamar #yemen #iran
5 Jul 2025
- Doctors have credited the 'folds' with playing a crucial role in one's hearing.
5 Jul 2025
- Gachagua said this during her aunt's burial ceremony.
5 Jul 2025
- ODM was responding to The Standard Media's 'Raila's Turf Rebels' article.
6 Jul 2025
- Traders affected by the recent demonstrations held in honour of victims of last year’s anti-Finance Bill protests are now struggling to rebuild their lives and livelihoods.
6 Jul 2025
- Deputy President Kithure Kindiki and other leaders backing the broad-based government have intensified attacks on the opposition, calling for unity to heal the nation.
6 Jul 2025
- The High Commission of Rwanda in Kenya has marked 31 years of liberation — a commemoration of the country’s remarkable transformation, from a painful past under an oppressive regime to a future defined by unity, progress, and resilience.
5 Jul 2025
- Opposition leaders have come out guns blazing to condemn President William Ruto's stance on constructing a church within the State House precincts, using what the president describes as his own money.
5 Jul 2025
- A family in Eldoret, Uasin Gishu County, is mourning the loss of their son, Timothy Bwibo, who succumbed to gunshot injuries on Friday night.
5 Jul 2025
- Former Meru Governor Kawira Mwangaza has been named the new party leader of Umoja na Maendeleo Party, taking over from Charles Wambora Mugambi.
5 Jul 2025
- National Assembly Speaker Moses Wetang’ula has faulted the trend of tribal and divisive politics, cautioning that such narratives risk plunging the country into dangerous polarization.
5 Jul 2025
- President William Ruto has replaced former Kesses Member of Parliament Dr. Swarup Mishra as the chair of the Kenya BioVax Institute, three months after suspending him.
5 Jul 2025
- James McMurdock denies any wrongdoing over claims relating to pandemic-era loans taken out by his companies.
5 Jul 2025
- Kenya’s road to the 2025 World Athletics Championships in Tokyo enters a decisive phase on Saturday, July 5, 2025, as the Prefontaine Classic in Eugene, Oregon, doubles as the national trials for the women’s 5,000m and men’s 10,000m races. While reigning…