Mwili wa Mtanzania uliyozama Wapatikana Mto wa Miami
Mwili uliopatikana ukielea katika Mto wa Miami Jumanne asubuhi umethibitishwa kuwa wa mtu mmoja aliyeanguka ndani ya maji kutoka katika boti wikiendi.
Mwili huo ulipatikana katika mto karibu na daraja moja lilioko katika eneo la 300 block huko Kaskazini magharibi 2nd Street.
Kanda ya video iliyochukuliwa kutoka katika helikopta aina ya Chopper 6 ilionyesha boti ya uokoaji ya Kikosi cha Zimamoto cha Miami kikishughulikia kuuopoa mwili huo kutoka majini.
Maafisa wa Polisi wa Miami wamethibitisha mwili huo kuwa wa Abraham Mgowano, aliyetoweka tangu Jumamosi mchana.
Mgowano mwenye umri wa miaka 35, alikuwa mfanyakazi wa Google, katika nafasi ya uhandisi ambaye Gazeti la The Citizen la Tanzania limeripoti kuwa marehemu ni mwenye asili ya Tanzania.
Kulingana na Kamisheni ya Florida Fish and Wildlife Conservation FWC, Mgowano kutoka Berkley, California, alikuwa ni moja wa abiria 12 katika boti iliyo na urefu wa futi 44, kabla ya kuanguka majini kiasi cha saa nane na nusu mchana.
Waokoaji kutoka Zimamoto ya Miami waliutafuta mwili wa mtu huyo aliyekuwa na umri wa miaka 35 aliyeanguka majini.
Kikosi cha Ulinzi wa Majini cha Marekani kilijiunga na zoezi hilo la kumtafuta mtu huyo lakini walisitisha utafutaji wao Jumamosi usiku.
Maafisa wa Kamisheni (FWC) walisema Jumatatu kuwa walikuwa wanaendelea kushirikiana na Polisi wa Miami-Dade na Waokoaji wa Kikosi cha Zimamoto cha Miami kutafuta mwili katika eneo hilo.
Maafisa wa FWC pia wamethibitisha kuwa mwili huo ni wa Mgowano na walisema uchunguzi bado unaendelea.
“Mioyo yetu iko na marafiki na familia ya Bw Mgowano wakati huu mgumu unaowakabili,” FWC ilisema katika taarifa yao.
#mwili #marehemu #abrahammgowano #miami #florida #marekani #voa #voaswahili #fwc
12 Aug 2025
- The Kenyan is expected in Nairobi on Sunday.
12 Aug 2025
- The bank will be created before the year ends.
12 Aug 2025
- The drivers were told to suspend their trip until further notice.
12 Aug 2025
- The agreement was reached during the 7th Session of the Kenya–Iran Joint Commission for Cooperation (JCC) held in Nairobi, co-chaired by Prime Cabinet Secretary Musalia Mudavadi and Iran’s Minister of Agricultural Jihad, Dr. Gholamreza Nouri Ghezalcheh.
12 Aug 2025
- The Ethics and Anti-Corruption Commission (EACC) has recovered public land in Kakamega valued at Ksh.20 million belonging to the Ministry of Housing.
12 Aug 2025
- Senior Principal Magistrate Dolphina Alego dismissed the request, ruling that Khatwani had failed to present sufficient justification for the release of his travel document, which is currently held in court as part of his bail conditions in a Sh356…
12 Aug 2025
- Dagoretti North MP Beatrice Elachi has called for more stringent and unpredictable checks on public servants’ wealth declarations, saying the current system is easily circumvented and ineffective in fighting corruption.
12 Aug 2025
- The Kenyan is expected in Nairobi on Sunday.
12 Aug 2025
- The bank will be created before the year ends.
12 Aug 2025
- The drivers were told to suspend their trip until further notice.
12 Aug 2025
- The High Court on Tuesday dismissed a petition challenging the appointment of PSC Vice Chairperson Mary Kimonye and commissioners Boya Molu, Irene Asienga, and Francis Meja.
12 Aug 2025
- The deal will solve a diplomatic fallout between the two countries.
12 Aug 2025
- According to a police report filed at Kehancha Police Station under OB No. 7/10/8/2025, Corporal James King’ori Karimi, attached to DCI Kuria West, discovered his pistol missing in the early hours of Sunday morning.