Mwili wa Mtanzania uliyozama Wapatikana Mto wa Miami
Mwili uliopatikana ukielea katika Mto wa Miami Jumanne asubuhi umethibitishwa kuwa wa mtu mmoja aliyeanguka ndani ya maji kutoka katika boti wikiendi.
Mwili huo ulipatikana katika mto karibu na daraja moja lilioko katika eneo la 300 block huko Kaskazini magharibi 2nd Street.
Kanda ya video iliyochukuliwa kutoka katika helikopta aina ya Chopper 6 ilionyesha boti ya uokoaji ya Kikosi cha Zimamoto cha Miami kikishughulikia kuuopoa mwili huo kutoka majini.
Maafisa wa Polisi wa Miami wamethibitisha mwili huo kuwa wa Abraham Mgowano, aliyetoweka tangu Jumamosi mchana.
Mgowano mwenye umri wa miaka 35, alikuwa mfanyakazi wa Google, katika nafasi ya uhandisi ambaye Gazeti la The Citizen la Tanzania limeripoti kuwa marehemu ni mwenye asili ya Tanzania.
Kulingana na Kamisheni ya Florida Fish and Wildlife Conservation FWC, Mgowano kutoka Berkley, California, alikuwa ni moja wa abiria 12 katika boti iliyo na urefu wa futi 44, kabla ya kuanguka majini kiasi cha saa nane na nusu mchana.
Waokoaji kutoka Zimamoto ya Miami waliutafuta mwili wa mtu huyo aliyekuwa na umri wa miaka 35 aliyeanguka majini.
Kikosi cha Ulinzi wa Majini cha Marekani kilijiunga na zoezi hilo la kumtafuta mtu huyo lakini walisitisha utafutaji wao Jumamosi usiku.
Maafisa wa Kamisheni (FWC) walisema Jumatatu kuwa walikuwa wanaendelea kushirikiana na Polisi wa Miami-Dade na Waokoaji wa Kikosi cha Zimamoto cha Miami kutafuta mwili katika eneo hilo.
Maafisa wa FWC pia wamethibitisha kuwa mwili huo ni wa Mgowano na walisema uchunguzi bado unaendelea.
“Mioyo yetu iko na marafiki na familia ya Bw Mgowano wakati huu mgumu unaowakabili,” FWC ilisema katika taarifa yao.
#mwili #marehemu #abrahammgowano #miami #florida #marekani #voa #voaswahili #fwc
8 May 2024
- The duo also detailed how the new trend can be addressed.
8 May 2024
- The Ministry will award the amount as capital grants to State Agencies and other levels of government to spearhead the initiative.
8 May 2024
- The Kenya Defence Forces are expected at the scene with sniffer dogs.
8 May 2024
- Two fishermen in Suba North constituency, Homa Bay County have drowned in Lake Victoria after engaging in a physical confrontation over a fish breeding zone in the lake.
8 May 2024
- The Council of Governors (COG) has called for the establishment of a dedicated fund to finance infrastructure projects in cities and towns affected by floods.
8 May 2024
- The Ministry of Health has embarked on an exercise that will see a combined effort between the two levels of government to pay close attention to internally displaced persons camps to combat diseases that may arise from the prolonged rains.
8 May 2024
- Twenty families who were living near a three-storey building in Kutus town, Kirinyaga County were forced to vacate on Tuesday night after the apartment under construction developed cracks.
8 May 2024
- Zimbabwe's treasury said on Tuesday the newly introduced gold-backed currency is the official unit of exchange for transactions and that it would soon introduce regulations to ensure businesses stick to the official rate.
8 May 2024
- All occupants of 5-storey apartment that collapsed in Uthiru accounted for; Red Cross says
8 May 2024
- Justice Sifuna stated that such could not be granted on mere fere and paranoia.
8 May 2024
- Reading Time: 3 minutes Bumula MP Wamboka Wanami yesterday disclosed that he will write to donor partners to request them to declare embattled Agriculture […]
8 May 2024
- Wheels of Justice: Court stories lined up for today.
8 May 2024
- The CS says there are new threats in the region as floods leave trail of death.