Kuporomoka kwa daraja kuu la Baltimore, watu 20 watafutwa
Kikosi cha uokoaji na utafutaji kina endelea na zoezi la kuwatafuta watu 20 waliotoweka baada ya daraja kuu kubomoka katika mji wa Baltimore, Maryland ulioko kusini mwa Marekani
Video iliyochukuliwa kwa simu ya mkononi ilionyesha vipande kadhaa vya Daraja la Scott Key likiporomoka ndani ya maji ya Mto Patapsco baada ya meli iliyobeba mizigo yenye bendera ya Singapore inayoitwa Dali kugonga nguzo inayoshikilia daraja majira ya saa kumi na moja alfajiri (05:30 UTC) Jumanne.
Mamlaka zinasema magari kadhaa yalikuwa juu ya daraja wakati ajali hiyo ilipotokea.
Maafisa wa huduma za dharura wa Baltimore kikosi cha watafutaji na waokoaji kinaendelea kuwatafuta watu wasiopungua 20 ambao wanasadikiwa kuwa ndani ya maji.
Magari kadhaa yalianguka kwenye maji baridi na waokoaji walikuwa wakitafuta zaidi ya watu saba.
Wanasema vyombo vyao vimebaini kuna magari yaliyotumbukia mtoni.
Inaonekana Meli hiyo iligonga nguzo moja ya daraja Fransis scott key Bridge ambapo lilivunjika vipande, kulingana na picha zilibandikwa katika mtandao wa X.
Meli hiyo ilisababisha moto ulitoa moshi mweusi ulopaa hewani.
Meli hiyo inayosafiri na bendera ya Singapore na jina la Dali ilikuwa imeondoka bandarini dakika 25 zilizopita ikielekea Singapore.
Synergy Marine Corp, Wasimamizi wa meli ya Dali, wametoa taarifa wakisema meli hiyo iligonga moja ya nguzo za daraja hilo na kuwa mabaharia wake wote, wakiwemo nahodha wa meli hiyo wamesalimika na hakuna ripoti zozote za majeruhi.
Daraja hilo lenye urefu wa kilomita 2.5 lenye umri wa miaka 47 ni kiungo kikuu katika njia kuu zinazounganisha majimbo zinazo zunguka mji wa Baltimore, moja ya bandari kadhaa kubwa kabisa za Marekani.
Ilipewa jina la Francis Scott Key, mwandishi wa “The Star Spangled Banner,” shairi ambalo baadae lilitengenezwa kuwa muziki na hatimaye kuwa ni nyimbo ya taifa ya Marekani.
Key alihamasishwa kuandika shairi baada ya kushuhudia mashambulizi ya bomu yaliyofanywa na Uingereza katika ngome kuu ya jeshi la Marekani huko Baltimore mwaka 1814. - VOA NEWS, AP, Reuters
#Daraja #baltimore #kubomoka #magari #mtoni #francisscottkeybridge #marekani
9 May 2024
- Real estate experts often advise Kenyans to visit areas they would want to live in when it rains to best assess the living conditions. Here is where to start.
9 May 2024
- The request came in and contradicted earlier reports made to the UN.
9 May 2024
- The police officer became disgruntled after both of his wives left their matrimonial home following the dispute.
10 May 2024
- The leader of Yemen's Houthis, Abdul Malik al-Houthi, said on Thursday the group would target ships of any company related to supplying or transporting goods to Israel regardless of their destination.
10 May 2024
- Stormy Daniels returned to the witness stand on Thursday at Donald Trump's historic hush money trial with attorneys for the former president seeking to paint her as a greedy liar who profited from her allegations.
10 May 2024
- Israeli tanks and warplanes bombarded areas of Rafah on Thursday, Palestinian residents said, after U.S. President Joe Biden vowed to withhold weapons from Israel if its forces launch a major invasion of the southern Gaza city.
10 May 2024
- Civilian contractors have arrived in Haiti to build living quarters for a Kenyan-led international security force meant to counter gang violence in the Caribbean nation, the U.S. military's Southern Command said.
10 May 2024
- Somalia's government has requested the termination of a U.N. political mission that has advised it on peace-building, security reforms and democracy for over a decade, according to a letter the foreign minister wrote to the Security Council.
10 May 2024
- Relatives of 44 construction workers trapped under a collapsed building in the South African city of George faced a fourth day of anguished waiting on Thursday as heavy machinery worked at the site in a race against time to find any survivors.
10 May 2024
- State to use Sh300m to settle flood victims
10 May 2024
- More than 1,600 schools not ready for learning
10 May 2024
- Riggy G declares 'war' on Marigiti brokers, I can only wish him well in his endeavours
10 May 2024
- Kemsa won't supply drugs to counties over Sh3b debt