Wanajeshi 8 DRC wahukumiwa kifo kwa kukimbia vita
Mahakama ya kijeshi katika mji wa Goma huko Kivu Kaskazini Mashariki mwa Congo imewahukumu kifo maafisa nane wa jeshi la Congo, FARDC kwa tuhuma za kukimbia vita na kutoheshimu sheria za kijeshi.
Miongoni mwao ni Kanali Shamba mkuu wa kikosi cha makomandoo pamoja na msaidizi wake.
Mwendesha mashtaka amesema makamanda hao walishindwa kuwajibika kwenye uwanja wa mapambano karibu na mji wa Sake wilayani Masisi eneo lililo magharibi mwa mji wa Goma ambako M23 wanaendelea kuchukua udhibiti wa vijiji.
Wakili wa makamanda hao Bwito Jean Richard wa jeshi tiifu kwa serikali amesema mahakama imefanya makosa kutoa adhabu ya kifo kwa wanajeshi hao ambao walikuwa wamejitolea kulipigania taifa.
Hata hivyo amekata rufaa na kuionya Mahakama kuwa makini kwa kuwa hatua za mahakama zinaweza kuwapelekea wanajeshi wengi kutokwenda vitani.
Lakini baadhi ya wachambuzi wamesema hatua hii itawazuia wanajeshi kukimbia mapigano kila mara na kuwaacha waasi kuchukua vijiji.
Katika hukumu hiyo wanajeshi watatu, kapteni mmoja na maluteni wawili waliachiliwa huru na mahakama kwa madai ya kutokuwa na hatia.
Makamanda hao walipewa adhabu ya kifo kwa mujibu wa sheria ya nchi hiyo. Wakati huohuo Mkuu wa mahakama ameziomba pande husika kukata rufaa katika kipindi cha siku tano.
#mahakama #kijeshi #wanajeshi #hukumu #kifo #vita #voa #voaswahili #mahakamayakijeshi
Imeandaliwa na Austere Malivika , Sauti ya Amerika Goma
11 Aug 2025
- Special trade agreements between Kenya and the UK allow the export of both goods and labour.
11 Aug 2025
- This comes a day after the case was reported at the Capitol Hill Police Station.
11 Aug 2025
- KUPPET claims that TSC should follow in the footsteps of the National Police Service.
11 Aug 2025
- Colombian presidential candidate Miguel Uribe has died two months after being shot at a campaign rally, his family said Monday, as the attack rekindled fears of a return to the nation's violent past.
11 Aug 2025
- Speaking when he commissioned classrooms and a water Project, Funyula, Busia County, Mudavadi, the former DP was a bitter person who had spent his entire time on his US tour planting tribalism abroad.
11 Aug 2025
- The head of a powerful Tunisian trade union confederation called on Monday to defend the group after protesters backed by President Kais Saied levelled harsh accusations against it.
11 Aug 2025
- Kenya and the U.S. state of California are strengthening cooperation in technology, climate innovation, and sustainable development, President William Ruto announced on Monday.
11 Aug 2025
- Fresh fighting between the Somali government and forces loyal to the semi-autonomous southern Jubaland region killed at least two Somali soldiers on Monday, the defence ministry said.
11 Aug 2025
- Data shows accidents have claimed 2,933 this year, with 80 deaths occurring over the past four days.
11 Aug 2025
- Justice Bahati Mwamuye issued the directive after lawyer Kibe Mungai, representing the petitioner, informed the court that the DPP had yet to file his response, stalling progress in the case.
11 Aug 2025
- He said DJ Fatxo, who was linked to the death, was his mentee.
11 Aug 2025
- Seeing a young man happily walking arm in arm with an older woman in Nairobi streets is common.
11 Aug 2025
- This follows a decision by US Congress to review of Kenya’s designation as a major non-NATO ally.