- 669 viewsDuration: 2:59Wakulima wa mahindi katika maeneo tofauti wanakadiria hasara kubwa kutokana na mvua inayoendelea kunyesha katika sehemu nyingi humu nchini. Hali hiyo imesababisha mavuno kuozea mashambani huku wakulima wakisalia kutazama jasho lao likiambulia patupu. Na Kama anavyoarifu Collins Shitiabayi, wakulima huko Trans nzoia sasa wanaitaka serikali iwasaidie na mashine za kukausha mahindi bila malipo na kuongeza bei ya mahindi kuwa angalau shilingi 3000 kwa gunia la kilo 50.