- 12,073 viewsDuration: 5:02Askofu mkuu mstaafu wa kanisa katoliki jimbo la Kisumu Zacchaeus Okoth amemuomboleza hayati Raila Odinga kama mtu aliyekuwa mwepesi wa kusamehe na aliyeweka taifa kabla ya maslahi yake. Okoth aliyekuwa miongoni mwa viongozi wa dini walioongoza maombi katika uwanja wa Jomo Kenyatta Mamboleo, huko kisumu kabla ya wananchi kuruhusiwa kuuona mwili wake Raila alisifia juhudi za Raila zilizosababisha kupatikana kwa katiba mpya, akisema mabadiliko nchini yalipatikana kupitia jasho na machozi ya Raila Amollo Odinga.