- 673 viewsNdugu na jamii ya mwanariadha aliyevunja rekodi ya dunia Kelvin Kiptum huko katika Kaunti ya Elgeyo Marakwet walikusanyika nyumbani kwa nyota wa riadha Jumatatu kuifariji familia yake baada ya kusikia habari za kifo chake kilichotokana na ajali ya gari. Baba yake alilia na kughubikwa na hisia wakati alipokuwa ameketi pamoja na waliokuja kuomboleza. Samson Cheruyot, mkulima, alisema Kiptum alitarajia kubadilisha hali ya familia yake kwa umaarufu alioupata ghafla, na walikuwa wamezungumzia kujenga nyumba na kuipatia familia yake gari. “Hivi sasa sijui niseme nini; hivi sasa kila mmoja ananiangalia mimi, hatujui tufanye nini,” Cheruyot alisema. Mkewe, Asenath Cheruto Rotich, alisema kuwa Kiptum alikuwa ni baba mwenye mapenzi kwa watoto wake. Rotich alisema alikuwa na wasiwasi kuhusu maisha ya watoto wao wawili na kuiomba serikali kumsaidia. “Ninaiomba serikali inisaidie ili niweze kuwasaidia watoto hawa kama baba yao alivyokuwa anawasaidia. Alikuwa anawapenda watoto wake, sijui hata kile ambacho nitawaambia,” alisema. Ilikuwa wiki chache zilizopita Kiptum aliapa kuvunja rekodi yake mwenyewe ya dunia kuwa mwanariadha wa kwanza kumaliza mbio za marathon chini ya saa mbili katika mashindano yajayo ya Rotterdam mwezi Aprili, na pia kujitokeza kwa mara ya kwanza katika mashindano ya Olimpiki huko Paris kipindi cha joto. Ndoto hiyo imekufa Jumapili wakati baba huyo wa watoto wawili mwenye umri wa miaka 24 alipofariki akiwa pamoja na kocha wake katika ajali ya gari huko Rift Valley. Polisi ilisema mwanariadha huyo alipoteza udhibiti wa gari alilokuwa analiendesha na kuacha njia akitumbukia katika shimo, akiwa amesafiri umbali wa takriban kilomita 0.06 kabla ya kugonga mti mkubwa. #Kenya #Kelvin #Kiptum #death #family #mourn #VOAAfrica
Baba, Mke na Wanafamilia wamlilia Hayati Kiptum
- 5 Jul 2025 - The Orange Democratic Movement (ODM) has slammed media reports which claimed that the party leader, Raila Odinga, is losing popularity in his backyard of Nyanza due to the events that unfolded during the burial of late teacher Albert Ojwang' at Kakoth…
- 5 Jul 2025 - The Judicial Service Commission (JSC) has strongly condemned what it terms as excessive use of force by police officers during the re-arrest of youth politician Peter Kinyanjui, alias Kawanjiru within the Ruiru Law Courts, saying the actions undermine…
- 5 Jul 2025 - Former Deputy President Rigathi Gachagua has launched scathing accusations against President William Ruto, claiming the Head of State is systematically persecuting the Mt. Kenya community.
- 5 Jul 2025 - Royal Media Services was on Friday night recognized as one of the top community promoters of road safety in Kenya.
- 5 Jul 2025 - Former Meru Governor Kawira Mwangaza has officially become the new leader of the Umoja na Maendeleo Party (UMP). This announcement was made public by the Office of the Registrar of Political Parties (ORPP) through a gazette notice, which confirmed she is…
- 5 Jul 2025 - Former Public Service Cabinet Secretary Justin Muturi has chided politicians for misusing the term honourable. Speaking on Saturday, July 5, 2025, during the burial of Gachagua’s aunt in Nyeri County, the former AG stated that the honorary title should…
- 5 Jul 2025 - Chinese firm tasked with managing the road, has filed at least 65 cases to recover the money it spends on repairing damage from accidents.
- 5 Jul 2025 - Democracy ensures the 'right people' get the mandate to instill fear in us. This fear should be moderated by justice. That is the work of the government and its institutions.
- 5 Jul 2025 - National chair Gladys Wanga reaffirmed Raila’s status as a towering national figure.
- 5 Jul 2025 - “The church serves the 1,000+ government staff and their families who live in State House.” Ndii said.