Bei ya Petroli, Dizeli na Mafuta Taa yashuka

  • | Citizen TV
    4,178 views

    Ni afueni zaidi kwa wakenya baada ya mamlaka ya kudhibiti bidhaa za kawi na petroli kutangaza kushuka kwa bei za petorili, dizeli na mafutaa taa kwa mwezi mmoja ujao. Katika tangazo lililotolewa leo na katibu Mkuu wa mamlaka ya EPRA, bei ya mafuta ya petroli imepunguzwa kwa shilingi tano na senti 31. Dizeli imepunguzwa kwa jumla ya shilingi kumi huku wateja wa mafuta ya taa wakipata afueni kubwa kwani lita moja ya bidhaa hiyo imepungua kwa shilingi kumi na nane na senti sitini na nane. Jijini Nairobi, Petroli sasa itauzwa shilingi 193 na senti themanini na nne kwa kila lita huku dizeli ikiuzwa shilingi 180 na senti thelathini na nane na mafuta ya taa itauzwa shilingi 170 na senti sita. Mjini Mombasa petrol itauzwa shilingi 190 na senti sitini na sita huku mjini nakuru, bei ikiwa shilingi 192 na senti tisaini. Mkurugeniz mkuu wa EPRA David Kiptoo amesema wakenya watazamie kupungua kwa gharama ya umeme hivi karibuni.