Skip to main content
Skip to main content

Eliud Owalo azindua chama kipya cha kisiasa

  • | Citizen TV
    205 views
    Duration: 1:00
    Aliyekuwa Waziri wa Habari na Teknolojia, Eliud Owalo, amezindua chama cha kisiasa kitakachobeba azma yake ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao. Owalo amesema chama chake cha Peoples Prosperity Party (PPP) kitajikita katika kuimarisha uchumi wa taifa, kufanya mageuzi ya ushuru, kukuza ustawi wa michezo na kuhakikisha utekelezaji wa Katiba. Aidha, amesema serikali zilizopita zimeshindwa kushughulikia ipasavyo changamoto zinazowakabili Wakenya na kwamba chama chake kinatoa mbadala wa uongozi.