Skip to main content
Skip to main content

Familia ya kijana aliyeuawa Urusi yazika mti baada ya kukosa mwili

  • | Citizen TV
    2,753 views
    Familia zaidi zimeendelea kujitokeza kuelezea namna jamaa zao walivyouawa au kupotea baada ya kusafiri kuelekea nchini Urusi kwa ajira. Vijana wapatao 15 kutoka vijiji kadhaa vya eneo la Transmara wakiwa kati ya wale walioondoka nchini kupigana vita vya urusi na hadi leo hawajulikani waliko. Katika eneo la Bonchari kaunti ya Kisii, familia ya kijana Clinton Nyapara aliyeripotiwa kuuawa akiwa vitani imezika mti baada ya kukata tamaa ya kupata mwili wa jamaa yao