- 4,314 viewsDuration: 4:52Je, wawakumbuka Kapenguria 6? Miongoni mwao alikuwa marehemu Ramogi Achieng' Oneko—shujaa wa uhuru ambaye mchango wake uliweka msingi wa safari ya uhuru wa Kenya . Miaka kumi na tisa baada ya kifo chake, familia yake sasa yadai kuwa fidia ya shilingi milioni kumi ambayo iliahidiwa kwa shujaa huyo wa uhuru haikuwahi kumfikia, licha ya serikali kuthibitisha kuwa waliokuwa wamezuiliwa pamoja na familia zao wangepokea fidia hiyo.