Familia za vijana waliouawa wakati wa maandamano ya mwaka jana wakabiliwa na maafisa wa polisi

  • | Citizen TV
    5,879 views

    Familia za vijana waliouawa wakati wa maandamano ya mwaka jana walikabiliwa na gesi ya kutoa machozi walipokuwa wakishiriki maandamano ya amani kuwakumbuka wapendwa wao. Miongoni mwa waliokabiliwa na tukio hilo ni jamaa za marehemu na watetezi wa haki akiwemo aliyekuwa Jaji Mkuu David Maraga. Matumizi haya ya nguvu bila ya kuchokozwa yameibua ukosoaji mkubwa, hasa ikizingatiwa kuwa kulikuwa na ahadi kwamba familia hizo zingetengewa mazingira salama ya kuomboleza bila tatizo.