[[Bassirou Diomaye Faye aliapishwa Jumanne kuwa rais mpya wa Senegal. Faye alimshinda mpinzani wake mkuu na mgombea wa muungano wa chama tawala Amadou Ba na kumshinda kwa kupata zaidi ya 54% ya kura katika uchaguzi uliocheleweshwa. ]]
Bassirou Diomaye Faye aliapishwa Jumanne kama rais wa tano wa Senegal katika Ukumbi wa Kimataifa wa CICAD uliopewa jina la rais wa pili wa nchi hiyo, uliopo eneo la Diamniadio, kiasi cha umbali wa saa moja kutoka mjini Dakar.
Rais mpya wa Senegal amesema: “Mbele ya Mungu na taifa la wasenegal, naapa kuwa nitatekeleza majukumu ya rais wa Jamhuri ya Senegal kwa uaminifu, na kuwa nitafuata kikamilifu na kuhakikisha natekeleza vifungu vyote vya katiba na sheria mbalimbali.”
Katika hotuba yake ya kwanza baada ya sherehe za kuapishwa, Rais Faye aliwahakikishia wananchi waliomchagua kuwa yuko tayari kuipeleka nchi mbele. - VOA
#rais #senegal #upinzani #BassirouDiomayeFaye #sherehe #kuapishwa #voa #voaswahili
2 May 2024
- Nairobi Governor Johnson Sakaja is under fire over the county’s response to floods from the heavy rainfall being experienced across the country.
2 May 2024
- A formal request has been issued to the United States Speaker of the House of Representatives and Republican member of Congress Mike Johnson; for President William Samoei Ruto to address a joint session of Congress.
2 May 2024
- Police tore down a protest encampment at the University of Texas on Wednesday, arresting more than a dozen people, as unrest over Israel's war against Hamas in Gaza simmered on US campuses.