- 6,699 viewsDuration: 2:49Kinara wa DCP Rigathi Gachagua sasa anasema ni yeye tu ndiye mwenye misuli kamili kumwondoa Rais William Ruto debeni mwaka ujao. Gachagua akisema kuwa anaamini ana uungwaji mkono zaidi ya vinara wengine wa upinzani kusimama dhidi ya Rais Ruto na kutwaa ushindi. Hata hivyo amewarai viongozi wenzake wa upinzani kutafuta uungwaji mkono kote nchini kabla hawajaketi mezani kuamua atakayepeperusha bendera.