- 21,912 viewsDuration: 3:08Aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua sasa anasema atakata rufaa kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ulioidhinisha kutimuliwa kwake afisini na Senate of Kenya, akisema uamuzi huo ulikuwa mapinduzi ya Katiba. Gachagua, aliyetoa taarifa kwa vyombo vya habari leo, aidha alitangaza kwamba atachukua likizo fupi ya kisiasa ya siku 45 kujadili suala la nani atakuwa mgombea wa urais wa muungano wa upinzani, akisisitiza kwamba yeye pia atakuwa debeni.