- 2,018 viewsDuration: 1:17Gavana wa Nairobi na Mwenyekiti wa Kamati ya Utekelezaji wa Mkataba wa Ushirikiano, Sakaja Johnson, ameamuru maandalizi ya mpango wa kushughulikia athari za mafuriko jijini ndani ya saa 48. katika mkutano uliohudhuriwa na makatibu wakuu wa serikali kuu, Sakaja amewaamuru maafisa wa serikali kuandaa ripoti ya ramani ya maeneo yenye maji mengi, kutambua barabara na miundombinu iliyoharibiwa, kuelezea kazi inayohitajika, mashirika yanayohusika, na gharama ili ukarabati uanze mara moja.