- 2,267 viewsDuration: 1:53Gavana wa Kaunti ya Kwale Fatuma Achani amezindua rasmi ujenzi wa barabara tatu za cabro katika wadi za Ukunda Bongwe Gombato na gatuzi dogo la Msambweni. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Gavana Achani amesema miradi hiyo inalenga kuboresha mji wa kitalii wa Diani ili kuvutia watalii na wawekezaji zaidi katika eneo hilo na kukuza uchumi wa Kaunti ya Kwale kupitia kuimarishwa kwa miundomsingi.