- 1,009 viewsDuration: 4:16Hali ya taharuki imetanda katika eneo la mlima Kilimapesa huko Transmara Kusini, eneo ambalo ni maarufu kwa madini ya dhahabu, maelfu ya wenyeji walisitisha shughuli zao za uchimbaji wa madini kulalamikia madai ya baadhi ya mabwenyenye kutaka kuwafurusha na kuendeleza biashara ya madini. Wakazi wanasema hawatakubali mwekezaji kutoka ughaibuni na wanasaisa kuhusishwa kuendeleza shughuli za uchimbaji wa madini eneo hilo..