- 2,332 viewsDuration: 2:36Aliyekuwa waziri mkuu mwendazake Raila Odinga alianza safari yake ya mwisho kutoka nairobi mapema asubuhi ya Jumamosi, mwili wake ukisafirishwa kutoka makafani ya Lee hadi kituo cha jeshi la angani cha Embakasi. Marehemu Raila akisafirishwa hadi Kisumu kwa ndege maalum, iliyoondoka mwendo wa saa 6:30 asubuhi. Familia ya mwendazake waliandamana na mwili katika ndege hiyo, maafisa wa kijeshi wakisafiri kwa ndege nyingine.