Israel yaendeleza vita dhidi ya Hamas na Islamic Jihad
Jeshi la Israeli limetoa kanda ya video Jumatano (Julai 10) ikionyesha kile walichosema ni majeshi ya ardhini yakifanya operesheni Gaza wakati mashauriano ya kusitisha mapigano katika vita vilivyodumu kwa miezi tisa yamepangwa kuanza tena.
Jeshi la Israeli lilisema katika taarifa yake kuwa majeshi yake yalikuwa yanaendelea na operesheni huko Gaza City dhidi ya wanamgambo wa Hamas na washirika wao Islamic Jihad, ambao walisema walikuwa wanafanya mashambulizi kutoka katika kituo cha UNRWA, wakikitumia kama ni ngome yao ya kufanya mashambulizi.
Kulingana na jeshi la Israeli walikuwa wamefanyia operesheni zao katikati mwa Gaza na Shejaiya.
Shirika la habari la Reuters halikuweza kuthibitisha eneo linaloonyeshwa katika kanda ya video. Reuters imeshindwa kupata uthibitisho huru wa tarehe ambayo video hiyo ilichukuliwa.
Vita hiyo ilianza Oktoba 7 wakati wapiganaji kutoka Palestina wa kikundi cha wanamgambo wa Hamas walipovamia mpakani na kushambulia jamii mbalimbali huko Israel, ikiuwa watu 1,200 na kuwateka watu 250, kulingana na idadi iliyotolewa na Israeli.
Shambulizi la Israeli huko Gaza kulipiza kisasi lilianza siku hiyo hiyo kwa kushambulia kwa mabomu na limeendelea kwa miezi tisa pamoja na uvamizi wa ardhini ambapo mamlaka za afya Palestina zinasema imeuwa zaidi ya watu 38,000 na kujeruhi zaidi ya watu 80,000.
Idadi kubwa ya waliojeruhiwa kutokana na vita hivyo imeongeza magonjwa kusambaa na utapiamlo kati ya wakazi asilimia 90 wa Gaza ambapo Umoja wa Mataifa unasema wamekoseshwa makazi, na kuweka shinikizo kubwa kwa mifumo ya afya katika eneo hilo finyu. - Reuters
#Rafah #Netanyahu #Misri #Hamas #Gaza #Palestina #IDF #GalMeirEizenkot #mauaji #jeshi #israel #voa #voaswahili #mwandishi #aljazeera #maghazi #wahouthi #marekani #uingereza #shambulizi #dhamar #yemen #hospitali #nasserhospital
13 May 2025
- This is not the first time a petition is being filed against the DCJ.
13 May 2025
- Kimani Ichung'wah, who has been receiving criticism from Kenyans, has asked for forgiveness.
13 May 2025
- The latest report highlights a paradigm shift from the traditional income-generating investments to value-driven luxuries.
14 May 2025
- Sean "Diddy" Combs' former girlfriend, Casandra Ventura, the star prosecution witness at the hip-hop mogul's sex trafficking trial, testified on Tuesday that her music career began to suffer as she increasingly spent her time participating in days of…
14 May 2025
- South Africa's unemployment rate rose in the first quarter of this year, with statisticians fretting that increasing numbers of people appear to have given up looking for work.
14 May 2025
- Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu said the military will enter Gaza "with full force" in the coming days, despite ongoing ceasefire efforts and the release of a US-Israeli hostage from the war-ravaged territory.
14 May 2025
- Finland President Alexander Stubb has hailed the historical Kenyan Gen Z movement witnessed in June last year during the anti-government protests, saying it was a momentous display of democracy.
14 May 2025
- Opposition leaders are now claiming that the Independent Electoral and Boundaries Commission (IEBC) nominees presented to Parliament for approval to take up management of the electoral body are a project to rig the 2027 General Election.
14 May 2025
- The crisis in the country's education sector continues to deepen, with the latest development being a Ksh.62 billion budget shortfall.
14 May 2025
- Tanzanian authorities arrested a senior opposition official as he was departing for a political conference in Belgium, his party said on Tuesday, as fears grow of an escalating crackdown ahead of an October election.
14 May 2025
- “No clean water. No toilets. No electricity. No well-planned living environment.” That is how Pastor Evans Moseti describes the one-room mabati house he has called home for the past nine years, its blue iron-sheet walls barely holding back Nairobi’s…
14 May 2025
- CBK rejects banks' rate cap claims, digs in on Ruto's loan reforms
14 May 2025
- How current political ongoings might affect various 'kingpins'