Ivory Coast Yaibuka Kidedea Fainali ya AFCON 2023
Sebastien Haller alifunga bao la ushindi dakika tisa kabla ya mchezo kumalizika wenyeji Ivory Coast wakinyakua taji la tatu la Kombe la Mataifa ya Afrika kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Nigeria kwenye mchezo wa fainali Uwanja wa Alassane Ouattara mjini Abidjan Jumapili (Februari 11).
Ni ushindi ambao haungetarajiwa na wengi siku chache zizlizopita hasa kutokana na kwamba timu hiyo ilipata vipigo viwili katika katika awamu ya makundi, kikiwemo kile cha mabao 4-0 kutoka kwa Equatorial Guinea, kabla ya kujizatiti katika raundi ya mchujo.
Bao la kichwa la William Troost-Ekong liliiwezesha Nigeria kuongoza kipindi cha kwanza lakini mchezaji machachari wa Ivory Coast, Franck Kessie alisawazisha.
Wenyeji Ivory Coast walilazimika kutoka nyuma mara kadhaa kwenye dimba hilo na walifanya hivyo tena wakati Haller alipoelekeza krosi ya Simon Adingra wavuni, jambo lililomfurahisha sana kocha wake Emerse Fae, ambaye alianza mchuano huo kama msaidizi wa Mfaransa Jean-Louis Gasset aliyetimuliwa.
Mafanikio ya Ivory Coast yanawafanya kuongeza taji la mwaka huu kwa mengine waliyoyapata mwaka wa 1992 na 2015, wakati ushindi huu pia unawaruhusu kuungana na Nigeria kwa ushindi wa tatu wa Kombe la Mataifa kwa jumla.
Ni Misri, Cameroon na Ghana pekee ambazo zimeshinda taji hilo mara nyingi zaidi.
Ivory Coast imekuwa nchi mwenyeji wa kwanza kushinda AFCON tangu 2006.
- Reuters
#afcon #totalenergiesafcon2023 #soccer #football #africa #news #voaafrica
24 Jan 2025
- Janet Mbugua is a household name in Kenya's media industry due to her professional approach to her job as a news anchor.
24 Jan 2025
- Gachagua's case was adjourned in November last year after he filed another case at the Appellate Court.
24 Jan 2025
- Wairimu is set to appear in court on Friday to respond to the fresh charges.
24 Jan 2025
- Wiper Party Leader Kalonzo Musyoka has criticised the government’s alleged decision to withdraw the security detail of Chief Justice Martha Koome, demanding the immediate reinstatement of her bodyguards.
24 Jan 2025
- A Kilifi law court has surprised two Italians accused in a Ksh.32 million fraud case after ruling that it has jurisdiction to hear and determine the case.
24 Jan 2025
- A federal judge blocked Donald Trump's attempt to restrict birthright citizenship in the United States on Thursday as liberal states scored their first victory against the new president's hardline agenda.
24 Jan 2025
- US President Donald Trump will reach out to Kim Jong Un again, he said in an interview aired Thursday, calling the North Korean leader with whom he previously met three times a "smart guy."
24 Jan 2025
- Three people among them two women were killed by suspected bandits along the Tot-Koloa road in Elgeyo Marakwet County on Thursday evening.
24 Jan 2025
- Two women were shot dead by suspected bandits along the Tot-Koloa road in Elgeyo Marakwet County on Thursday evening.
24 Jan 2025
- A total of 546 bags of contraband rice impounded at a store in Eldoret town had failed the aflatoxin test. The angry youth wanted the rice distributed to them.
24 Jan 2025
- Hundreds of schools in Hungary received bomb threats on Thursday, officials said, forcing them to briefly evacuate students.
24 Jan 2025
- I am writing this article while listening to the legendary Kenny Rogers’ song “The Gambler”. This classic hit is more than just music; it is a reservoir of wisdom from which Kenyan politicians can draw. The song’s plot revolves around life lessons…
24 Jan 2025
- Janet Mbugua is a household name in Kenya's media industry due to her professional approach to her job as a news anchor.