Jaji mkuu Koome atetea uhuru wa mahakama

  • | Citizen TV
    628 views

    Jaji Mkuu Martha Koome ametetea uhuru wa idara ya mahakama akisema kamwe haitayumbishwa na shutuma kuhusu utendakazi wake. Koome akitoa hakikisho kuwa majaji wataendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia katiba. Jaji Mkuu amezungumza haya huku shutuma zikiendelea kuhusu baadhi ya maamuzi yake haswa kwa dhamana ya washukiwa wa maandamano