Joseph Irungu akata rufaa dhidi ya hukumu ya kifo

  • | Citizen TV
    2,795 views

    Mtuhumiwa wa mauaji Joseph Irungu maarufu kama jowie amekata rufaa kuhusu hukumu ya kifo aliyopewa na jaji grace nzioka baaada ya kupatikana na hatia ya kumuua mfanyibiashara monica kimani. Jowie anasema kuwa hukumu hiyo iliyotolewatarehe 13 mwezi Machi inakiuka haki zake za kikatiba. anataka mahakama kuagiza kuwa hukumu ya kifo ni ya kinyama na kikatili na inakiuka katiba.jowie pia anapinga kanuni za kesi za jinai zinazomzuia mtuhumiwa wa mauaji kupewa dhamana akisubiri rufaa. Jowie pia anataka kufidiwa akisema haki zake za kimsingi zimekiukwa.