- 767 viewsDuration: 1:45Katibu wa chama cha UDA Hassan Omar amelaumu upinzani kwa kile anachodai kuwa wamekuwa wakimshambulia rais na matusi kwa muda akisema ndio chanzo cha majibizano machafu yalioshuhudiwa. Akizungumza huko Mombasa wakati wa kikao na wamachama wa UDA Omar ametaka upinzani kukoma kueneza siasa chafu na kuwagawanya wakenya. Viongozi kutoka UDA wamepinga hoja ya chama ODM kutaka nafasi ya naibu wa rais wakisema wanamuunga mkono Kithure Kindiki.